Sunday, April 17, 2016

Enyi watu wa mataifa yote msifuni BWANA kwa maana fadhili zake ni za milele na milele. Tunamshukuru MUNGU kwa matendo yake makuu juu ya maisha yetu ibada ya leo ameonekana kwa namna ya kipekee. Ni ibada ambayo pia  iliambatana na changizo fupi kwa ajili ya uzinduzi wa Album mpya ya Hope kwaya ambao uzinduzi wake utafanyika 24/04/2016. Katika changizo hili washarika pamoja na uongozi wa CCT walishirikiana kwa pamoja kufanikisha tukio hilo katika ibada ya leo.Yafuatayo ni baadhi ya matukio ambayo yalitukia katika ibada ya leo
Mchungaji kiongozi Canon Nyagawa akihudumu katika Ibada

Keki kwa ajili ya tukio la changizo ikiandaliwa na viongozi wa kamati ya uzinduzi

Washarika wakisikiliza neno la BWANA

Keki imekwisha andaliwa kwa ajili ya changizo
Mzee wa kanisa akisoma Matangazo

Praise and worship team wakihudumu katika Ibada
MUNGU AISHIYE MILELE AWABARIKI WOTE WALIOSHIRIKI KATIKA IBADA KWA MATOLEO, CHANGIZO  NA PIA WALIOFIKA KUIANDAA IBADA HII.

No comments:

Post a Comment